Maandalizi ya Moyo: Heart Preparation.
BY: RAYMOND ANTONY.
“Hakuna madhihirisho pasipokuwa na maandalizi”
“There is no manifestation without preparation…”
Mit 16:1“Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.”
Siku zote neno la mwenye moyo safi hupokelewa na Mungu. Hivyo moyo ni eneo muhimu linalopaswa kuandaliwa kabla ya kwenda kukutana na Mungu. Kwa lugha rahisi, moyo ni madhabahu itumikayo kuweka sadaka iliyo safi mbele za Bwana.
Maandalizi makubwa ya moyo, huleta madhihirisho makubwa.
taz. (1fal 18:21-29) “…Kwa hiyo na watutolee ng’ombe wawili; wao na wajichagulie ng’ombe mmoja, wamkate-kate na kumweka juu ya kuni, wasitie moto chini; nami nitamtengeneza huyo ng’ombe wa pili, na kumweka juu ya kuni, wala sitatia moto chini. Nanyi ombeni kwa jina la mungu wenu, nami nitaomba kwa jina la BWANA; na Mungu yule ajibuye kwa moto, na awe ndiye Mungu. ….. wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeneza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri…. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu, wala aliyeangalia.”
Mdahalo huu, baina ya Eliya na manabii wa Baali, ulikuwa unahitaji kuonyesha uwezo wa mungu ambaye aliaminika ana nguvu kutoka kila upande, yaani Mungu wa Eliya au mungu Baali. Hivyo maandalizi yalihitajika ili kufanikisha adhma zao.
Kwa upande wa manabii wa Baali walioanza walifanya maandalizi yao “….wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa wakamtengeneza,…” Maandalizi yao yaliangalia zaidi ile sadaka iliyotolewa (ng’ombe) kuliko madhabahu.
Kwa upande wa Eliya nabii wa Mungu aliye hai alijiandaa namna hii; taz (1waf 18:30-35) “…Kisha Eliya akawaambia watu wote, nikaribieni mimi. Watu wote wakamkaribia. Akaitengeneza madhabahu ya BWANA iliyovunjika. Eliya akatwaa mawe kumi na mawili, kwa hesabu ya kabila za wana wa Yakobo,…Naye akaijenga madhabahu kwa mawe hayo katika jina la BWANA; akafanya mfereji, kama wa vipimo viwili vya mbegu, ukiizunguka madhabahu. Kisha akazipanga zile kuni,akamkata yule ng’ombe vipande vipande, akaviweka juu ya kuni…”
Maandalizi makubwa ya moyo (madhabahu) huleta madhihirisho makubwa na ushindi. Eliya aliweza kumwabudu Mungu na kumtukuza mbele ya manabii wa Baali, baada ya kukamilisha madhabahu aliyokuwa akiiandaa. Taz (1waf 18:36-39)
Mungu hushuka na kupokea sadaka ya mioyo yetu, kama kuna maandalizi mazuri ya moyo. Katika agano la kale, sadaka ilitolewa juu ya madhabahu iliyojengwa.
Taz (mwa 22:9) “wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kasha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.”
Kama ilivyoelezewa hapo juu, leo mioyo yetu imefanyika kuwa madhabahu, inayobeba maombi na sifa za Mungu, maana maombi na sifa ni sehemu ya dhabihu au sadaka kati ya nyingi mbele za bwana.
Kitu kinachochipuka kutoka ndani ya moyo, huwa hakisahauliki na hakipotezi ladha yake. Huwa kina nguvu ya pekee.
Mara nyingi wanadamu wamekuwa wakiangalia mwonekano wa nje, lakini Mungu hutazama ndani ya mioyo ya watu.
No comments:
Post a Comment